<?xml version="1.0" encoding="UTF-8"?>
<rss version="2.0"
	xmlns:content="http://purl.org/rss/1.0/modules/content/"
	xmlns:wfw="http://wellformedweb.org/CommentAPI/"
	xmlns:dc="http://purl.org/dc/elements/1.1/"
	xmlns:atom="http://www.w3.org/2005/Atom"
	xmlns:sy="http://purl.org/rss/1.0/modules/syndication/"
	xmlns:slash="http://purl.org/rss/1.0/modules/slash/"
	xmlns:itunes="http://www.itunes.com/dtds/podcast-1.0.dtd"
	xmlns:media="http://search.yahoo.com/mrss/"
>

<channel>
	<title>IPS - TerraViva World Social Forum 2011 &#187; Swahili</title>
	<atom:link href="http://www.ips.org/TV/wsf/category/swahili/feed/" rel="self" type="application/rss+xml" />
	<link>http://www.ips.org/TV/wsf</link>
	<description>During 2011, IPS-TerraViva reports from many of the thematic and geographic forums planned throughout the year</description>
	<lastBuildDate>Fri, 25 Mar 2011 11:58:44 +0000</lastBuildDate>
	<language>en</language>
	<sy:updatePeriod>hourly</sy:updatePeriod>
	<sy:updateFrequency>1</sy:updateFrequency>
	<generator>http://wordpress.org/?v=3.0.4</generator>
	<copyright>Copyright &#xA9; IPS - TerraViva World Social Forum 2011 2011 </copyright>
	<managingEditor>nacho@ips.org (IPS - TerraViva World Social Forum 2011)</managingEditor>
	<webMaster>nacho@ips.org (IPS - TerraViva World Social Forum 2011)</webMaster>
	<image>
		<url>http://www.ips.org/TV/wsf/wp-content/plugins/podpress/images/powered_by_podpress.jpg</url>
		<title>IPS - TerraViva World Social Forum 2011</title>
		<link>http://www.ips.org/TV/wsf</link>
		<width>144</width>
		<height>144</height>
	</image>
	<itunes:subtitle></itunes:subtitle>
	<itunes:summary>During 2011, IPS-TerraViva reports from many of the thematic and geographic forums planned throughout the year</itunes:summary>
	<itunes:keywords></itunes:keywords>
	<itunes:category text="Society &#38; Culture" />
	<itunes:author>IPS - TerraViva World Social Forum 2011</itunes:author>
	<itunes:owner>
		<itunes:name>IPS - TerraViva World Social Forum 2011</itunes:name>
		<itunes:email>nacho@ips.org</itunes:email>
	</itunes:owner>
	<itunes:block>no</itunes:block>
	<itunes:explicit>no</itunes:explicit>
	<itunes:image href="http://www.ips.org/TV/wsf/wp-content/plugins/podpress/images/powered_by_podpress_large.jpg" />
		<item>
		<title>Wanawake na Watoto wa ‘Afrika’ Ni Waathirika Wakuu wa Migogoro</title>
		<link>http://www.ips.org/TV/wsf/wanawake-na-watoto-wa-%e2%80%98afrika%e2%80%99-ni-waathirika-wakuu-wa-migogoro/</link>
		<comments>http://www.ips.org/TV/wsf/wanawake-na-watoto-wa-%e2%80%98afrika%e2%80%99-ni-waathirika-wakuu-wa-migogoro/#comments</comments>
		<pubDate>Fri, 11 Feb 2011 14:30:09 +0000</pubDate>
		<dc:creator>admin</dc:creator>
				<category><![CDATA[Swahili]]></category>
		<category><![CDATA[WSF 2011]]></category>
		<category><![CDATA[Africa]]></category>
		<category><![CDATA[human rights]]></category>
		<category><![CDATA[Liberia]]></category>
		<category><![CDATA[Mama]]></category>
		<category><![CDATA[Rwanda]]></category>
		<category><![CDATA[Sierra Leone]]></category>
		<category><![CDATA[war]]></category>
		<category><![CDATA[Winston]]></category>
		<category><![CDATA[women]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://www.ips.org/TV/wsf/?p=2941</guid>
		<description><![CDATA[Mmoja wa mabinti wanaoongoza Afrika na mwanaharakati wa haki za wanawake, mwanazuoni wa Nigeria Amina Mama anasema wanamgambo wanaopigana wanaenea hasa katika nchi za Sierra Leone na Liberia.]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<p>Na Thandi Winston</p>
<p>DAKAR, Feb 11 (TerraViva) – Mmoja wa mabinti wanaoongoza Afrika na mwanaharakati wa haki za wanawake, mwanazuoni wa Nigeria Amina Mama anasema wanamgambo wanaopigana wanaenea hasa katika nchi za Sierra Leone na Liberia. Anasema vita na migogoro inaathiri wanawake ambao ni rahisi kuathirika pamoja na watoto wao.<span id="more-2941"></span></p>
<div id="attachment_2848" class="wp-caption alignleft" style="width: 220px"><a href="http://www.ips.org/TV/wsf/library/20110209_QAMama_KristinPalitzaIPS.jpg"><img class="size-medium wp-image-2848  " title="20110209_QAMama_KristinPalitzaIPS" src="http://www.ips.org/TV/wsf/library/20110209_QAMama_KristinPalitzaIPS-300x198.jpg" alt="Rape survivor in Malawi's Dzaleka camp for Congolese refugees: every month, seven to ten cases of gender-based violence are reported; few perpetrators are brought to justice. Credit: Kristin Palitza/IPS" width="210" height="139" /></a><p class="wp-caption-text">Rape survivor in Malawi&#39;s Dzaleka camp for Congolese refugees: every month, seven to ten cases of gender-based violence are reported; few perpetrators are brought to justice. Credit: Kristin Palitza/IPS</p></div>
<p>Mama alikuwa akiongea na IPS pembezoni mwa Kongamano la Kijamii la Dunia kuhusu kuenea kwa wanamgambo wanaopigana katika bara na mjadala wa wanaharakati wa masuala ya wanawake katika kongamano la mwaka huu.</p>
<p>“Wanawake na watoto wamekuwa waathirika wakuu wa migogoro, iwe ile ya baada ya ukoloni au isiwe hiyo, nina imani maslahi ya makampuni yamechochea migogoro,” alisema.</p>
<p>Ukiukwaji wa haki za binadamu unaofanywa dhidi ya wanawake wakati wa migogoro umekuwa mkubwa mno. Utafiti wa mwaka 1999 nchini Rwanda kama sehemu ya Mfuko wa Kimataifa wa Wanawake  (GFW) katika mpango wa Kuenea kwa Mapigano ya Wanamgambo, unasema asilimia 39 waliripoti kubakwa wakati wa mauaji ya kimbari mwaka 1994. Asilimia sabini na mbili walisema walijua mtu ambaye alibakwa.</p>
<p>Katika sampuli iliyochukuliwa bila mpangilio maalum ya wakimbizi wanawake 388 wa Liberia wanaoishi katika makambi nchini Sierra Leone, robo tatu waliripoti kudhalilishwa kingono kabla ya kukimbia makazi yao nchini Liberia. GFW ilikuta kuwa zaidi ya nusu walifanyiwa vitendo vya udhalilishaji wa kingono tangu walipokimbia.</p>
<p>Wastani wa wanawake 50,000 hadi 64,000 walioyakimbia makazi yao walilengwa kudhalilishwa kingono wakati wa vita nchini Sierra Leone.</p>
<p>Mama, ambaye ni mhariri mwanzilishi wa jarida la wanazuoni la harakati za kijinsia la kwanza barani Afrika, ‘Feminist Africa’, kwa sasa ni wenyekiti wa Mfuko wa Kimataifa wa Wanawake, ambao unatoa ruzuku kwa mashirika yanayopigania haki za wanawake duniani kote.</p>
<p>“Kumekuwepo na mabadiliko juu ya kudumu kwa migogoro na vita katika baadhi ya maeneo ya Afrika,” anasema, “Mabadiliko haya yanasababisha aina maalum ya sera na ufuatiliaji na unyanyasaji dhidi ya wanawake. Yanajikusanya jinsi muda unavyosogea.</p>
<p>“Kongo ni mfano mmojawapo, kama ukiangalia unyanyasaji na ubakaji, ulianza wakati wa ukoloni wa Ubelgiji. Hivi ndivyo wanavyofanya kazi.</p>
<p>“Na leo hii wanaume wameiga utamaduni huo wa kutumia vita waliojifunza kutoka kwa wakoloni wa Magharibi.”</p>
<p>Mama kwa sasa anafanya kazi na wanaharakati wa wanawake wa Nigeria, Sierra Leone na Liberia ili kujenga ufahamu wa madhara ya vita kwa wanawake na watoto.</p>
<p>(END/2011)</p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://www.ips.org/TV/wsf/wanawake-na-watoto-wa-%e2%80%98afrika%e2%80%99-ni-waathirika-wakuu-wa-migogoro/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>1</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Lula na Wade Katika Kona Mkabala</title>
		<link>http://www.ips.org/TV/wsf/lula-na-wade-katika-kona-mkabala/</link>
		<comments>http://www.ips.org/TV/wsf/lula-na-wade-katika-kona-mkabala/#comments</comments>
		<pubDate>Fri, 11 Feb 2011 07:00:33 +0000</pubDate>
		<dc:creator>admin</dc:creator>
				<category><![CDATA[Swahili]]></category>
		<category><![CDATA[WSF 2011]]></category>
		<category><![CDATA[Fórum Social Mundial]]></category>
		<category><![CDATA[liberalismo]]></category>
		<category><![CDATA[Lula]]></category>
		<category><![CDATA[Wade]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://www.ips.org/TV/wsf/?p=2919</guid>
		<description><![CDATA[Dhana ya uliberali iliyoanzishwa katika nchi maskini zaidi haina nafasi katika jamii za kisasa, anasema rais wa zamani wa Brazili, Luiz Inácio Lula da Silva.]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<p>Na Koffigan E. Adigbli</p>
<p>DAKAR, Feb 11 (TerraViva) – Dhana ya uliberali iliyoanzishwa katika nchi maskini zaidi haina nafasi katika jamii za kisasa, anasema rais wa zamani wa Brazili, Luiz Inácio Lula da Silva.<span id="more-2919"></span><br />
Lula, kama ambavyo anajulikana zaidi, alijitokeza pamoja na Rais wa Senegal Abdoulaye Wade katika Kongamano la Kijamii la Dunia mjini Dakar, ambapo anashiriki katika mkutano wa wanaharakati wa kudai dunia mbadala kutoka duniani kote. Lula alitoa hotuba ambapo alionyesha kuwa na matumaini juu ya takwimu za kiuchumi za sasa.</p>
<div id="attachment_2720" class="wp-caption alignleft" style="width: 310px"><a href="http://www.ips.org/TV/wsf/library/20110208_Lula_AbdullahVawdaIPS.jpg"><img class="size-medium wp-image-2720" title="20110208_Lula_AbdullahVawdaIPS" src="http://www.ips.org/TV/wsf/library/20110208_Lula_AbdullahVawdaIPS-300x214.jpg" alt="Brazilian president Luiz Inácio Lula da Silva. Crédit: Pepo Petos/WSFTV" width="300" height="214" /></a><p class="wp-caption-text">Brazilian president Luiz Inácio Lula da Silva. Crédit: Pepo Petos/WSFTV</p></div>
<p>“Mfumo wa kiuchumi duniani sasa hautajengwa tena na nchi chache zenye uchumi mkubwa,” alisema.</p>
<p>“Katika Amerika Kusini, lakini zaidi ya hapo katika mitaa ya Tunis na Cairo na miji mingi katika mataifa mengine mengi ya Afrika, matumaini mapya yanazaliwa. Mamilioni ya watu wanaibuka kupingana na umaskini ambao unawakabili, dhidi ya kudhibitiwa na madikteta, dhidi ya nchi zao kukubaliana na sera za mataifa yenye nguvu duniani,” alisema Lula.</p>
<p>Pia alitoa wito kwa Afrika kutambua fursa katika bara hilo na mustakabali mzuri ambao unalisubiri bara hilo, lenye wakazi milioni 800 na utajiri wake mkubwa wa ardhi, ambao ungeruhusu kufikia uhuru wake wa uzalishaji wa chakula.</p>
<p>“Kwa muda mrefu, nchi tajiri zimetuona kama watu hatari na watu wenye matatizo, lakini wale ambao wametupatia masomo ya jinsi gani lazima tusimamie uchumi wetu tena kwa mbwembwe kubwa, hawajaweza wao wenyewe kuepuka mgogoro uliotokana na kitovu cha ubepari duniani,” alisema.</p>
<p>Kwa upande wake, Rais Wade kwa uwazi alijiwakilisha kama mtetezi wa uchumi huria. Alikwenda umbali wa kuonyesha kuwa hakubaliani na harakati dhidi ya utandawazi, hata kama anakubaliana nao juu ya wazo lao la kubadili dunia, jambo ambalo linamfanya kukubaliana na haja ya kuleta mabadiliko.</p>
<p>“Naunga mkono uchumi wa soko na wala siyo uchumi unaoongozwa na serikali ambao umeshindwa mahali pengine au karibu katika dunia nzima,” alisema, akiongeza kuwa kwa muda mrefu alikuwa akifanya kampeni ya kuwa na kiti cha Afrika katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.</p>
<p>“Nyie nyote ambao mko hapa kama mngeunga mkono dhana hiyo, Afrika ingekuwa tayari ina kiti katika Baraza la Usalama. Tangu mwaka 2000, nimekuwa nikifuatilia harakati zenu na bado – samahani kwa kuwa mkweli – nawauliza swali hili: mmefanikiwa katika kubadili dunia katika ngazi ya kimataifa?”</p>
<p>(END/2011)</p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://www.ips.org/TV/wsf/lula-na-wade-katika-kona-mkabala/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Vurugu Katika Ukumbi Wakati UCAD Ikifuta Hifadhi ya Vyumba</title>
		<link>http://www.ips.org/TV/wsf/vurugu-katika-ukumbi-wakati-ucad-ikifuta-hifadhi-ya-vyumba/</link>
		<comments>http://www.ips.org/TV/wsf/vurugu-katika-ukumbi-wakati-ucad-ikifuta-hifadhi-ya-vyumba/#comments</comments>
		<pubDate>Thu, 10 Feb 2011 23:46:47 +0000</pubDate>
		<dc:creator>admin</dc:creator>
				<category><![CDATA[Swahili]]></category>
		<category><![CDATA[WSF 2011]]></category>
		<category><![CDATA[Africa]]></category>
		<category><![CDATA[Sillah]]></category>
		<category><![CDATA[UCAD]]></category>
		<category><![CDATA[Winston]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://www.ips.org/TV/wsf/?p=2904</guid>
		<description><![CDATA[Siku ya kwanza ya mikutano na mijadala katika Kongamano la Jamii la Dunia imeandamwa na vurugu za kutafuta kumbi za mikutano.]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<p><strong>Na Thandi Winston na Ebrima Sillah</p>
<p>DAKAR, Feb 10 (TerraViva) – Siku ya kwanza ya mikutano na mijadala katika Kongamano la Jamii la Dunia imeandamwa na vurugu za kutafuta kumbi za mikutano.</strong><span id="more-2904"></span></p>
<div id="attachment_2682" class="wp-caption alignleft" style="width: 220px"><a href="http://www.ips.org/TV/wsf/library/20110207_VenueChaosUCAD_Edited.jpg"><img class="size-medium wp-image-2682 " title="20110207_VenueChaosUCAD_Edited" src="http://www.ips.org/TV/wsf/library/20110207_VenueChaosUCAD_Edited-300x256.jpg" alt="WSF organisers have set up tents to accommodate sessions. Credit: Abdullah Vawda/IPS" width="210" height="179" /></a><p class="wp-caption-text">Chuo Kikuu cha Cheikh Anta Diop (UCAD) Credit: Abdullah Vawda/IPS</p></div>
<p>Chanzo kutoka ndani ya kamati ya maandalizi ya WSF kiliiambia IPS kuwa Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Cheikh Anta Diop (UCAD) alifuta vyumba vilivyohifadhiwa kwa ajili ya Kongamano katika maeneo ya chuo hicho. Baada ya mijadala vyumba 40 tu vilipatikana kati ya vyumba vya semina 200 ambavyo hapo kabla vilihifadhiwa kwa ajili ya WSF, na kuanza kutumiwa na wanafunzi waliokuwa wakiendesha masomo yao ya darasani kama kawaida katika vyumba vingine.</p>
<p>“Kwa sasa tunajaribu kufunga mahema kwa ajili ya ukumbi, ili tuweze kufanyia semina,” chanzo hicho kilisema.</p>
<p>Kuna karibu mikutano elfu mbili iliyopangwa kufanyika wiki hii. Washiriki wa WSF wanaowasili katika maeneo ya chuo asubuhi hii walikuta vyumba vingi vikiwa na wanafunzi wanaohudhuria masomo yao.</p>
<p>Kikundi cha haki ya ardhi nchini Brazili kilijikusanya chini ya kivuli cha mti kufanya mjadala juu ya upokonyaji wa ardhi ya wananchi katika Brazili na Afrika. Wengine walitoa sauti zao nje ya jengo la utawala la chuo kikuu.</p>
<p>Mmoja wa waandamanaji, Chilean Carolos Morales, alisema, “Pengine mtu katika chuo hakupenda kongamano kwasababu hata wanafunzi wao wangepata masuala mengi mno kuhusu ubepari wa kisasa na jinsi gani wanapoteza rasilimali za nchi kutokana na uroho.”</p>
<p>Makundi yaliyokuwa yakifanya mijadala na uwasilishaji wa mada yalikuwa yakitafuta kumbi mbadala siku nzima, halafu yalijaribu jinsi yanavyoweza kuhabarisha watu juu ya wapi mikutano inafanyikia. Mikutano mingi ambayo hapo awali ilipangwa kufanyika leo imefutwa.</p>
<p>(END/2011)</p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://www.ips.org/TV/wsf/vurugu-katika-ukumbi-wakati-ucad-ikifuta-hifadhi-ya-vyumba/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Mapinduzi Siyo Jambo Dogo</title>
		<link>http://www.ips.org/TV/wsf/mapinduzi-siyo-jambo-dogo/</link>
		<comments>http://www.ips.org/TV/wsf/mapinduzi-siyo-jambo-dogo/#comments</comments>
		<pubDate>Thu, 10 Feb 2011 23:30:51 +0000</pubDate>
		<dc:creator>admin</dc:creator>
				<category><![CDATA[Swahili]]></category>
		<category><![CDATA[Top Story]]></category>
		<category><![CDATA[WSF 2011]]></category>
		<category><![CDATA[Africa]]></category>
		<category><![CDATA[Bunge la Mwananchi]]></category>
		<category><![CDATA[civil society]]></category>
		<category><![CDATA[Climate change]]></category>
		<category><![CDATA[Egypt]]></category>
		<category><![CDATA[gender]]></category>
		<category><![CDATA[Kenya]]></category>
		<category><![CDATA[NGO]]></category>
		<category><![CDATA[PACJA]]></category>
		<category><![CDATA[Tunisia]]></category>
		<category><![CDATA[Umoja Peace Village]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://www.ips.org/TV/wsf/?p=2897</guid>
		<description><![CDATA[Nyuma ya vichwa vya habari vya makongamano ya kijamii na maandamano ya kutumia nguvu, kupambana na ukandamizaji na kubadili dunia kunahitaji hatua endelevu zinazojikita katika jamii ya chini, kulingana na mwanaharakati wa haki ya kijamii wa Kenya.]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<p><strong>Andrea Lunt anamhoji Mwanaharakati wa Kenya ONYANGO OLOO</strong></p>
<p><strong>NEW YORK, Feb 10 (IPS/TerraViva) – Nyuma ya vichwa vya habari vya makongamano ya kijamii na maandamano ya kutumia nguvu, kupambana na ukandamizaji na kubadili dunia kunahitaji hatua endelevu zinazojikita katika jamii ya chini, kulingana na mwanaharakati wa haki ya kijamii wa Kenya.</strong><span id="more-2897"></span></p>
<p>Wakati Kongamano la Kijamii la Dunia mwaka huu likifanyika kikamilifu, IPS ilizungumza na Oloo, mwandishi, mfungwa wa kisiasa wa zamani na mratibu wa taifa wa WSF wa mwaka 2007, kuhusu nchi yake ya Kenya, maandamano yanayoendelea Kaskazini mwa Afrika na vuguvugu la kijamii duniani kote. Sehemu ya mahojiano inafuata.</p>
<div id="attachment_2760" class="wp-caption alignleft" style="width: 132px"><a href="http://www.ips.org/TV/wsf/library/20110208_QAOloo_OnyangoOloo.jpg"><img class="size-thumbnail wp-image-2760" title="20110208_QAOloo_OnyangoOloo" src="http://www.ips.org/TV/wsf/library/20110208_QAOloo_OnyangoOloo-122x150.jpg" alt="Courtesy of Onyango Oloo." width="122" height="150" /></a><p class="wp-caption-text">Courtesy of Onyango Oloo.</p></div>
<p>Swali: Umepata nini katika maandamano yanayojitokeza katika eneo zima la Afrika Kaskazini? Ni kwa nini yanajitokeza sasa na unaamini kuwa yanaweza kusambaa katika kanda nyingine katika bara?</p>
<p>Jibu: Ninahamasishwa na kuvutiwa na kile kinachojitokeza nchini Misri na Tunisia. Mapinduzi yanaongezeka, kinyume na matangazo ya vyombo vikuu vya habari, yanatofautiana mno na birika la chai linalochemka ghafla.</p>
<p>Kinachojitokeza leo hii katika Afrika Kaskazini ni ushahidi wa harakati, ushindi na kurejea nyuma ambako kumejitokeza kwa miongo mingi na ni chanzo cha migogoro mingi mno ya kijamii – bila kujali kukosekana kwa muunganiko kati ya uundwaji wa ubeberu wa uliberali wa kisasa na mahitaji makubwa ya demokrasia, haki ya kijamii, amani na jamii bora.</p>
<p>Mapinduzi kwa asili yake siyo bidhaa zinazozalishwa kutoka kiwandani ambazo zinaweza kusafirishwa katika mfumo wa “shinda nishinde” katika nchi nyingine. Hata hivyo, nguvu ya mfano inapaswa kuwa kichocheo kwa ajili ya harakati nyingine za ukombozi wa kitaifa katika Afrika nzima na Mashariki ya Kati.</p>
<p>Swali: Kwa maoni yako, ni vuguvugu gani za kijamii zinazojitokeza nchini Kenya wakati huu?</p>
<p>Jibu: Hili ni swali gumu, kama siyo vigumu kulijibu. Kwanza, mtu hawezi kuweka vuguvugu za kijamii katika aina yoyote ile ya ukiritimba wa “umuhimu” nchini Kenya. Jambo la pili, na kuwa muwazi zaidi,  vuguvugu la kijamii nchini Kenya bado kwa kiasi kikubwa, ni dhaifu mno na wanaharakati wengi wako katika hatua ya uchanga.</p>
<p>Baadhi yao wamekamatwa na NGOs zinazopata ufadhili kutoka Magharibi ili ajenda zao zitekeleze vipaumbele vya wafadhili wa Amerika Kaskazini na mashirika ya wafadhili ya Ulaya.</p>
<p>Hata hivyo, naweza kutaja Bunge la Mwananchi kama shirika lililofanya kazi nzuri katika kusumbua hali ya ukoloni mamboleo.</p>
<p>Swali: Ni aina gani ya mafanikio au mifumo mbadala ya maendeleo nchini mwako, au katika Afrika kwa ujumla, ambayo yanaweza kuhamishiwa katika maeneo mengine ya dunia?</p>
<p>Jibu: Kuna maarifa mengi mno ya jadi ambayo mara nyingi “yanadhoofishwa” na vyombo vya habari vya Magharibi. Nazungumza kuhusu hifadhi ya maarifa ya jadi katika eneo la miti shamba na madawa ya jadi. Katika miaka michache iliyopita hata makampuni makubwa ya madawa yanakubali kuwa aina mbadala za afya ya jadi imeleta mifumo ya afya katika kushughulikia maladhi na magonjwa kama kisukari, magonjwa ya moyo, kansa ya kibofu, kifua kikuu na VVU/UKIMWI.</p>
<p>Rwanda imeonyesha njia ya kushughulikia amani na migogoro kupitia mahakama yake ya gacaca iliyoanzishwa baada ya mauaji makubwa ya kimbari katikati mwa miaka ya 1990.</p>
<p>Wakulima wa Afrika, kama ilivyo kwa wenzao wa Asia, wana njia bora zaidi za kuhifadhi mazingira na kuhifadhi maarifa ya mbegu tofauti na inavyofanya Monsantos ya dunia.</p>
<p>Kwa maoni yangu, wenzangu wa Kenya kutoka eneo linalozungumza lugha ya Maa wameonyesha ujasiri katika kushika utamaduni wao bila kuendeshwa na historia ya masalia yaliyohifadhiwa katika makumbusho.</p>
<div id="attachment_2759" class="wp-caption alignleft" style="width: 250px"><a href="http://www.ips.org/TV/wsf/library/20110208_QAOloo2_AdvocacyProject.jpg"><img class="size-medium wp-image-2759 " title="20110208_QAOloo2_AdvocacyProject" src="http://www.ips.org/TV/wsf/library/20110208_QAOloo2_AdvocacyProject-300x205.jpg" alt="Credit: Advocacy Project" width="240" height="164" /></a><p class="wp-caption-text">Umoja Peace Village. Credit: Advocacy Project</p></div>
<p>Wanawake wa Afrika, kama wanawake wa Umoja Peace Village karibu na Nanyuki katikati mwa Kenya, wamekuja na mifumo ya kuwapatia uwezo wanaharakati wa kijinsia unaotokana na ukweli halisi kama watu wa kijijini, makabila ya ufugaji ya watu wachache – mshtuko kwa wale ambao wana imani kuwa harakati za kijinsia Afrika zinatumika mijini, kwa ajili ya wanawake wenye elimu ya chuo kikuu.</p>
<p>Swali: Ni njia gani bora ya wanaharakati wa kijamii kufanya sauti zao kusikika na kuhakikisha kuwa mawazo yanayojadiliwa katika makongamano kama ya WSF yanatafsiriwa katika ukweli wa mabadiliko ya kisera katika ngazi za kitaifa na kimataifa?</p>
<p>Njia bora ya kufanya sauti zao kusikika siyo kusubiri matukio ya mwaka na vipindi vya Kongamano la Kijamii la Dunia. Tunazungumza vizuri kwa kuwa na ufahamu, tukiwa tumeungana, wenye nguvu na kuwa na hatua endelevu ya kisiasa katika ngazi ya mitaa, kitaifa na ngazi ya bara.</p>
<p>Ninachokisema kwa maneno mengine ni kwamba wanaharakati wasijikusanye tu mbele ya sauti nzuri za taarifa za habari za CNN, BBC, Al Jazeera au hata naweza kusema IPS, lakini kusikiliza dada zao na kaka wanaozungumza nao majumbani, katika jumuiya za mitaa na katika nchi zao wakati wakichambua na kujipanga kukabiliana na aina maalum ya ukandamizaji wao na changamoto.</p>
<p>Kwa njia hiyo, wakati wanaelekea maeneo kama Dakar na Porto Alegre, wenzao kutoka maeneo mengine ya dunia watakachotaka kusikia ni sauti zenye nguvu kutokana na harakati zao wenyewe nyumbani kwao.</p>
<p>Kwa bahati mbaya, sikwenda Dakar mwaka huu kwasababu sikuwa na fedha zozote zile za kupanda ndege kwenda Senegal. Wanaharakati wengi katika Afrika walikabiliwa na changamoto hii. Ni kumbukumbu ya kusikitisha ya vikwazo vinavyotokana na tabaka vya kushiriki katika matukio kama Kongamano la Kijamii la Dunia – hata kama yanafanyika katika bara ambalo tunaliita nyumbani.</p>
<p>(END/2011)</p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://www.ips.org/TV/wsf/mapinduzi-siyo-jambo-dogo/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Miaka 11 ya Migogoro Migumu Kutatua Kimataifa</title>
		<link>http://www.ips.org/TV/wsf/miaka-11-ya-migogoro-migumu-kutatua-kimataifa/</link>
		<comments>http://www.ips.org/TV/wsf/miaka-11-ya-migogoro-migumu-kutatua-kimataifa/#comments</comments>
		<pubDate>Thu, 10 Feb 2011 11:45:01 +0000</pubDate>
		<dc:creator>admin</dc:creator>
				<category><![CDATA[Swahili]]></category>
		<category><![CDATA[WSF 2011]]></category>
		<category><![CDATA[Dakar]]></category>
		<category><![CDATA[Porto Alegre]]></category>
		<category><![CDATA[RIO DE JANEIRO]]></category>
		<category><![CDATA[Senegal]]></category>
		<category><![CDATA[WSF]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://www.ips.org/TV/wsf/?p=2880</guid>
		<description><![CDATA[Uliberali wa kisasa na utandawazi wa kifedha ni maadui maarufu ambao waliunganisha na kukusanya wanaharakati ambao walianzisha, miaka kumi iliyopita mjini Porto Alegre kusini mwa Brazili, Kongamano la Kijamii la Dunia (WSF) kama nafasi ya kukutana, kutathmini na kujadili, chini ya kaulimbiu "Ulimwengu Mwingine Unawezekana".]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<p><strong>Mario Osava</strong></p>
<div id="attachment_2421" class="wp-caption alignleft" style="width: 280px"><strong><strong><a href="http://www.ips.org/TV/wsf/library/020411b.jpg"><img class="size-medium wp-image-2421 " title="020411b" src="http://www.ips.org/TV/wsf/library/020411b-300x225.jpg" alt="" width="270" height="203" /></a></strong></strong><p class="wp-caption-text">Credit: Ansel Herz/IPS</p></div>
<p><strong>RIO DE JANEIRO, Feb 10 (IPS) &#8211; Uliberali wa kisasa na utandawazi wa kifedha ni maadui maarufu ambao waliunganisha na kukusanya wanaharakati ambao walianzisha, miaka kumi iliyopita mjini Porto Alegre kusini mwa Brazili, Kongamano la Kijamii la Dunia (WSF) kama nafasi ya kukutana, kutathmini na kujadili, chini ya kaulimbiu &#8220;Ulimwengu Mwingine Unawezekana&#8221;.</strong><span id="more-2880"></span></p>
<p>Lakini katika miaka yake 11 tangu kuanzishwa, kongamano la WSF linakusanyika tena Feb. 6-11 mjini Dakar, Senegal, wakati ambapo uliberali wa kisasa, sera za soko huria vinasimama katika ulimwengu unaotishiwa na kuporomoka kutokana na mchanganyiko wa migogoro: ya kifedha, mabadiliko ya tabia nchi, chakula na maji.</p>
<p>Ubeberu wa Kimarekani, shabaha nyingine ya wanaharakati, umeshuhudia nguvu yake ya kiuchumi ikidhoofika wakati taifa jingine lenye nguvu, China, linaibukia na aina yake ya ukoloni, pamoja na kwamba haitumii mbinu za kijeshi au kusafirisha mfumo wake inaoamini na mtindo wake wa maisha – kwa sasa.</p>
<p>Kukua kwa nchi zinazoibukia kiuchumi kumefanya mamia kwa mamilioni ya watu kutoka kwenye umaskini mkubwa. Lakini kukosekana kwa usawa duniani na katika nchi moja moja bado ni doa, kama ilivyo kwa njaa inayokabili watu wengi katika pande nyingi za sayari.</p>
<p>Tishio la mabadiliko ya tabia nchi limeachwa kuongeza idadi ya watu waliokufa na kuhama makazi yao kutokana na matukio ya hali ya hewa, na kuongezeka kwa hasara inayotokana na kilimo.</p>
<p>Fedha zina nguvu kubwa ya kuangamiza, huku kukiwa na dola trilioni 860 zinazokadiriwa kuwa ni mtaji unaozunguka duniani kote – mara 13 zaidi ya Pato la Dunia la Mwaka – kulingana na “Bank of International Settlements”.</p>
<p>Yote hayo yanazidishwa na &#8220;utawala mbovu wa sayari&#8221; – kukosekana kwa taasisi zenye uwezo wa kushughulika na &#8220;matatizo ya kimataifa,&#8221; kulingana na mwanauchumi wa Brazili Ladislau Dowbor, ambaye anaelekea Dakar kubadilishana mawazo na kundi la wasomi ambao, chini ya jina la &#8220;Migogoro na Fursa&#8221;, wanajadili mifumo ya kiufumbuzi ya &#8220;mkusanyiko wa migogoro.&#8221;</p>
<p>Kuzidi kuongezeka kwa mkusanyiko wa utajiri mahali pamoja ambao umesababisha theluthi mbili ya binadamu kuondolewa katika maendeleo na kuishi kwa asilimia sita tu ya pato la dunia siyo suala endelevu, alisema Dowbor, profesa katika Chuo Kikuu cha Catholic São Paulo.</p>
<p>Wala haiwezekani kuendelea mbele katika &#8220;Mazingira haya Makubwa,&#8221; na kumaliza maliasili, &#8220;ardhi, viumbe wa baharini,&#8221; aliongeza.</p>
<p>Waraka muhimu wa kundi hilo la wasomi ambalo ni pamoja na Dowbor, na “mwanauchumi wa jamii” mwenye asili ya Poland na Ufaransa, Ignacy Sachs, na mwanauchumi na mpenda mageuzi wa Uingereza Hazel Henderson, unakataa &#8220;maono rahisi ya mchakato wa kutoa maamuzi ya kijamii,&#8221; unaotoa wito wa kuokoa &#8220;mwelekeo wa taifa la umma,&#8221; na kupendekeza kuondokana na GDP kama kiashiria kikuu cha uchumi, miongoni mwa mapendekezo mengine.</p>
<p>Kongamano la WSF linarejea Afrika katika awamu ya nane wakati maandamano ya raia yameshapindua serikali ya kidikteta ya Tunisia na mengine yanatishia kufanya kama hivyo nchini Misri.</p>
<p>Kongamano la mwaka huu &#8220;litakuwa zuri, kwa kuwa na watu wapya,&#8221; lakini litafanyika katika mazingira hatari, &#8220;huku likipata tu theluthi moja ya bajeti iliyokadiriwa hapo kabla,&#8221; alisema mmoja wa waanzilishi wa WSF, Cándido Grzybowski, mkurugenzi wa Taasisi ya Uchambuzi wa Kiuchumi na Kijamii Brazili (IBASE).</p>
<p>Katika matukio mengi, kwa mfano, hakutakuwa na watu wanaotafsiri papo hapo.</p>
<p>Baadhi ya washiriki 50,000 wanatarajiwa kushiriki, moja ya tatu ya jumla ya waliojisajili katika kongamano lililopita, lililofanyika mwaka 2009 katika jiji la kaskazini mwa Brazili la Belém katika msitu wa Amazon. &#8220;Lakini takwimu hiyo inaweza kuongezeka mara mbili, kutokana na kuongezeka kwa watu kutoka bara la Ulaya,&#8221; Grzybowski ana matarajio.</p>
<p>Senegal ina idadi ya watu wachache zaidi mara 15 ikilinganishwa na Brazili, alisema Chico Whitaker, mwanzilishi mwingine wa WSF, ambaye alielezea kuwa asilimia 80 ya washiriki katika matukio haya mara nyingi wanatoka nchi mwenyeji.</p>
<p>Uwepo wa washiriki kutoka Amerika Kusini utakuwa mdogo, kwa sehemu kutokana na matatizo ya kifedha yanayokabi mashirika yasiyokuwa ya kiserikali kutokana na kupungua kwa fedha za wafadhili, kulikozidishwa na viwango visivyokuwa vizuri vya ubadilishanaji wa fedha na uhaba wa ufadhili wa serikali za ndani. Na tiketi za ndege kwenda Dakar zinauzwa kwa gharama kubwa, kutokana na kukosekana kwa ndege za moja kwa moja kutoka Amerika Kusini; ndege zinapitia Ulaya.</p>
<p>Mapungufu ya maandalizi mjini Dakar yanaonyesha kukosekana kuungwa mkono na serikali, kutokana na msimamo uliochukuliwa na mmoja wa wanaharakati wa sasa wa Brazili ambaye aliandaa kongamano mwaka jana kaskazini mashariki mwa Brazili katika jimbo la Bahia na ambaye alitetea ushirikiano na serikali zenye maendeleo, kuimarisha matukio ya WSF na kuyafanya kuwa na faida kubwa.</p>
<p>Kongamano la WSF linafasiliwa kama mpango wa kijamii ambapo viongozi wa serikali wanashiriki tu kama wageni katika matukio yanayoandaliwa na wanaharakati na mashirika ya kijamii. Hata hivyo, makongmano mengi ya kijamii ya dunia, ikiwa ni pamoja nay ale matano yaliyofanyika nchini Brazili, wamepata msaada wa kifedha kutoka serikali za kitaifa au za mitaa.</p>
<p>Rais wa zamani wa Brazili Luiz Inácio Lula da Silva, mgeni mwalikwa katika makongamano yaliyopita, sasa atashiriki katika kongamano la Dakar kama &#8220;mjumbe kutoka mashirika ya kiraia &#8220;katika semina ya Jumamosi Feb. 7, siku ya Afrika na Waafrika Wanaoishi nje ya Bara katika ratiba ya WSF 2011.</p>
<p>Lula ametangaza kuwa mahusiano baina ya Brazili na Afrika itakuwa kipaumbele katika shughuli zake baada ya kuondoka serikalini.</p>
<p>Wabrazili wengi wanataka kurejesha WSF katika ukumbi wake wa zamani wa Porto Alegre, wakati wengine wanashinikiza kufanyika Bahia, jimbo lenye watu wengi wenye asili ya Afrika.</p>
<p>Lakini Ulaya, eneo jingine lenye nguvu linaloweza kuwa mwenyeji wa kongamano lijalo mwaka 2013, inajikita katika mifumo mingine, kama vile kujaribu kuwa na matunda katika masuala makubwa ya sasa.</p>
<p>Hata hivyo, ni mwelekeo mpya wa &#8220;dunia nyingine&#8221; ijayo, zaidi ya changamoto za sasa, ambazo zinatia wasiwasi kwa waanzilishi wa WSF. &#8220;Maendeleo ambayo yanaua maisha ya watu katika sayari ni tatizo kubwa,&#8221; alisema Grzybowski, ambaye alisema kuwa &#8220;uchumi wa kijani&#8221; kama ufumbuzi, akisema ni &#8220;ubepari uliotiwa kijani&#8221; ambao hauongezi tija katika mifumo ya mkakati huo.</p>
<p>Mapendekezo yake ni &#8220;kwenda zaidi ya WSF&#8221; na kutumia fursa ya Rio+20 ya mwaka kesho, Mkutano wa Umoja wa Mataifa wa Maendeleo Endelevu, ambao utaleta taarifa mpya zaidi na mjadala ulioanzishwa mwaka 1992 katika Mkutano wa Kilele wa Mazingira wa Rio de Janeiro.</p>
<p>Vuguvugu la kijamii linatakiwa kujipanga na kuwepo kwa wingi kwa wanaharakati katika mkutano wa mwaka 2012, ili kujenga ushirikiano na serikali ya Brazili kwa ajili ya kubadili jinsi mazingira na maendeleo yanapaswa kuwa, alisema.</p>
<p>Matatizo ya kimataifa ni mengi na magumu, lakini &#8220;dunia haiishii hapo, na watu wanapaswa kujenga historia,&#8221; kama inavyoonekana katika ulimwengu wa Waarabu katika siku chache zilizopita, alisema.</p>
<p>(END/2011)</p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://www.ips.org/TV/wsf/miaka-11-ya-migogoro-migumu-kutatua-kimataifa/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>&#8216;Ni Dalili za Mabadiliko&#8217; Asema Morales wa Bolivia Wakati wa Uzinduzi wa Kongamano</title>
		<link>http://www.ips.org/TV/wsf/ni-dalili-za-mabadiliko-asema-morales-wa-bolivia-wakati-wa-uzinduzi-wa-kongamano/</link>
		<comments>http://www.ips.org/TV/wsf/ni-dalili-za-mabadiliko-asema-morales-wa-bolivia-wakati-wa-uzinduzi-wa-kongamano/#comments</comments>
		<pubDate>Mon, 07 Feb 2011 12:22:24 +0000</pubDate>
		<dc:creator>admin</dc:creator>
				<category><![CDATA[Swahili]]></category>
		<category><![CDATA[WSF 2011]]></category>
		<category><![CDATA[Africa]]></category>
		<category><![CDATA[capitalism]]></category>
		<category><![CDATA[Egypt]]></category>
		<category><![CDATA[Faye]]></category>
		<category><![CDATA[gender]]></category>
		<category><![CDATA[Morales]]></category>
		<category><![CDATA[resource extraction]]></category>
		<category><![CDATA[Tunisia]]></category>
		<category><![CDATA[Winston]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://www.ips.org/TV/wsf/?p=2595</guid>
		<description><![CDATA[Makumi kwa maelfu ya watu waliandamana katika mitaa ya mji mkuu wa Senegal wa Dakar siku ya Jumapili kuashiria mwanzo wa Kongamano la Kijamii la Dunia linalofanyika kila mwaka. ]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<p><strong>Na Thandi Winston na Souleymane Faye*</strong></p>
<div id="attachment_2578" class="wp-caption alignright" style="width: 160px"><strong><strong><a href="http://www.ips.org/TV/wsf/library/20110206_MarcheALOuverture_AbdullahVawdaIPS.jpg"><img class="size-thumbnail wp-image-2578" title="20110206_MarcheALOuverture_AbdullahVawdaIPS" src="http://www.ips.org/TV/wsf/library/20110206_MarcheALOuverture_AbdullahVawdaIPS-150x150.jpg" alt="Kutoka kwa: Abdullah Vawda/IPS" width="150" height="150" /></a></strong></strong><p class="wp-caption-text">Kutoka kwa: Abdullah Vawda/IPS</p></div>
<p><strong>DAKAR, Feb 6  (IPS)  &#8211; Makumi kwa maelfu ya watu waliandamana katika mitaa ya mji mkuu wa Senegal wa Dakar siku ya Jumapili kuashiria mwanzo wa Kongamano la Kijamii la Dunia linalofanyika kila mwaka. Wanaharakati walibeba mabango ya rangi  mbalimbali yanayokemea upokonyaji wa ardhi, sheria kali za uhamiaji, ruzuku katika kilimo barani Ulaya na Marekani na masuala mengine mengi.<span id="more-2595"></span><br />
</strong><br />
Wengine waliimba nyimbo za uhuru na kupiga ngoma wakati wakiandamana kwa amani kupita katika mitaa kwenye njia inayoanzia karibu na ofisi za shirika la utangazaji la serikali ya Senegal, RTS, na kuishia katika Chuo Kikuu cha Cheikh Anta Diop, ukumbi mkubwa wa mkusanyiko huo.</p>
<p>Rais wa Bolivia Evo Morales, ambaye alishiriki katika maandamano, alikaribisha marais wenzake kutoka nchi maskini kushiriki katika tukio hilo.</p>
<p>&#8220;Ni lazima kuwepo na uhamasishaji ili kukomesha ubepari na kuwasafisha kabisa wavamizi, wakoloni mamboleo na mabeberu [...] naunga mkono maandamano ya raia nchini Tunisia na Misri. Hizi ni dalili za mabadiliko,&#8221; alisema Morales, kiongozi wa zamani wa chama cha wafanyakazi ambaye ni mshiriki wa mara kwa mara katika mikusanyiko ya harakati za kupinga utandawazi.</p>
<p>&#8220;Ni lazima kuwepo na upinzani na uhamasishaji. Ni lazima kuwepo na mpango wa harakati za kijamii kujenga dunia mpya,&#8221; alisema.</p>
<p>&#8220;Ni lazima kuokoa ubinadamu, na kwa kufanya hivyo, ni lazima kuwajua maadui wetu. Maadui wa watu ni wakoloni mamboleo na mabeberu. Ni lazima tukomeshe mfumo wa kibebari na kuweka mfumo mwingine katika nafasi yake. Ni vema kuondokana na matajiri na kubadili dunia.&#8221;</p>
<p>Meya wa jiji la Dakar alikaribisha washiriki, lakini wajumbe wengine waandamizi wa serikali ya Senegal hawakushiriki; Rais Abdoulaye Wade mwenyewe yuko nje ya nchi, pamoja na kwamba amepangwa kushiriki katika tukio hilo akiwa na mwenzake wa Brazili baadaye katika wiki.</p>
<p>Kongamano la Kijamii la Dunia linajifasili kama nafasi ya wazi ambapo wale &#8220;wanaopingana na uliberali wa kisasa na dunia inayoongozwa na mtaji au aina yoyote ile ya ubeberu wanakuja pamoja kutoa maoni yao.&#8221;</p>
<p>Katika tukio la mwaka huu lililofanyika mjini Senegal, mijadala mingi itajikita katika kile ambacho waandaaji wanakitaja kama mgogoro wa ustaarabu na ubepari unaoiandama Afrika na maeneo mengine ya dunia.</p>
<p>&#8220;Kongamano hili lazima lichangie katika kuibadili dunia. Ni fursa kwa wale wote ambao wanawakilisha wanaokandamizwa duniani kuzungumza sasa,&#8221; alisema mwanahistoria wa Senegal Boubacar Diop Buuba, ambaye ni profesa katika Chuo Kikuu cha Cheikh Anta Diop.</p>
<p>Philip Kumah, mfanyakazi wa kijamii nchini Ghana ambaye anafanya kazi katika shirika la Amnesty International, alisema, &#8220;Tunataka kukomeshwa kwa ukiukwaji wa haki katika nchi yetu ambayo serikali inawaibia wananchi ardhi. Kongamano hili ni nafasi kwa serikali zetu kuwa na sikio linalosikiliza malalamiko yetu.&#8221;</p>
<p>Kwa mwanaharakati Beverley Keene, kutoka Buenos Aires, kufanya kongamano hilo barani Afrika ni mwanzo muhimu. &#8220;Ni wakati wetu kujifunza kutoka kwa wengine na kutathmini madhara katika maisha ya jamii ambayo yametokana na mgogoro wa kifedha na uporaji wa madini ya wananchi.&#8221;</p>
<p>Mgogoro wa kifedha ni maarufu miongoni mwa kaulimbiu ambazo zitajadiliwa katika kongamano la siku sita ambalo linatafuta njia mbadala ya kukabiliana na &#8220;mgogoro uliotokana na mfumo wa kibepari.&#8221;</p>
<p>Mwanaharakati wa jinsia wa Italia Sabrina Viche alisema tukio hilo pia ni fursa ya kusikiliza wanawake wa Afrika. &#8220;Nimekuja hapa mjini Dakar kuunga mkono wanawake wote wa Afrika, ambao wanaendeleza harakati za kuhakikisha kuwa sauti zao zinasikika, nataka kusikia kutoka kwao harakati zao ni zipi na jinsi gani sisi wa Kaskazini tunaweza kuwasaidia.&#8221;</p>
<p>Lakini haijitoshelezi kukutana tu, Canet Raphael, mwanasosholojia kutoka Montréal, Canada, aliiambia IPS. &#8220;Lazima watu watambue kongamano la kijamii ni nini. Moyo wa Kongamano la Kijamii unatokana na mizizi kutoka vuguvugu la watu katika ngazi ya chini ya jamii.&#8221;</p>
<p>Thierry Tulasne, ambaye anafanya kazi inayohusu masuala ya uhamiaji kwenye shirika la Canada alisema, &#8220;Sina uhakika kuwa vuguvugu la kijamii linaweza kubadili dunia katika siku za karibuni. Lakini nina uhakika kwamba tone moja la maji linawezekana kuja kuwa mito mikubwa.&#8221;</p>
<p>(END/2011)</p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://www.ips.org/TV/wsf/ni-dalili-za-mabadiliko-asema-morales-wa-bolivia-wakati-wa-uzinduzi-wa-kongamano/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Kongamano la Kijamii la Dunia: Wakenya Wanawasha Moto Mwingine</title>
		<link>http://www.ips.org/TV/wsf/kongamano-la-kijamii-la-dunia-wakenya-wanawasha-moto-mwingine/</link>
		<comments>http://www.ips.org/TV/wsf/kongamano-la-kijamii-la-dunia-wakenya-wanawasha-moto-mwingine/#comments</comments>
		<pubDate>Sun, 06 Feb 2011 22:23:57 +0000</pubDate>
		<dc:creator>editor</dc:creator>
				<category><![CDATA[Swahili]]></category>
		<category><![CDATA[WSF 2011]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://www.ips.org/TV/wsf/?p=2569</guid>
		<description><![CDATA[“Miongoni mwa mambo ambayo tutayapeleka Dakar, anasema Onyango Oloo, “ni [ujuzi wa] kukosa uwezo wa kuandaa Kongamano la Jamii la Dunia.”]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<h2><span style="font-weight: normal; font-size: 13px;"></p>
<div id="attachment_2570" class="wp-caption alignleft" style="width: 310px"><a href="http://www.ips.org/TV/wsf/library/372.jpg"><img class="size-medium wp-image-2570 " title="37" src="http://www.ips.org/TV/wsf/library/372-300x199.jpg" alt="Paulino Menezes/IPS TerraVivaSherehe za Ufunguzi wa Kongamano la Kijamii la Dunia Mjini Nairobi. Kutoka kwa: Paulino Menezes/IPS TerraViva" width="300" height="199" /></a><p class="wp-caption-text">Paulino Menezes/IPS TerraVivaSherehe za Ufunguzi wa Kongamano la Kijamii la Dunia Mjini Nairobi. Kutoka kwa: Paulino Menezes/IPS TerraViva</p></div>
<p>Na Mary Itumbi</p>
<p></span></h2>
<p><strong>NAIROBI</strong><strong>, Feb 3 (IPS) – “Miongoni mwa mambo ambayo tutayapeleka Dakar, anasema Onyango Oloo, “ni [ujuzi wa] kukosa uwezo wa kuandaa Kongamano la Jamii la Dunia.” </strong><strong>Oloo alikuwa mratibu wa Kongamano la Jamii Duniani (WSF) lilipofanyika jijini Nairobi mwezi Januari 2007, na kuwa wa kwanza kugundua mikanganyiko  iliyoizunguka kongamano la kwanza la WSF kufanyika barani Afrika.<span id="more-2569"></span><br />
</strong></p>
<p>“Wakati huo huo tungependa kukumbuka kwamba Kongamano la Kijamii la Dunia lilikuwa kubwa kulikoni yote katika ardhi ya Kenya kuhusiana na uwakilishi wa jamii. Liliamsha hamasa nyingi, hata (kutoka) makundi mengine ya kijamii hususan mashoga, wasagaji, wanaopenda jinsi zote mbili, wanaharakati wote. Walizindua kwa mara ya kwanza, walisimika hema lao kubwa (katika eneo la kongamano) katika uwanja wa Karasani, mambo mengi ya kusisimua yalitokea.”</p>
<p>Zaidi ya watu 200 walihudhuria tukio la awali kabla ya WSF lililotayarishwa na shirika la kijamii la Nairobi Januari 29, kutoka vikundi mbalimbali vya mashirika yanayohusiana na masuala ya haki za binadamu, haki za wazawa, mabadiliko ya hali ya hewa na mengineyo. Tukio hilo lilifanyika katika Ukumbi wa Ufungamano, katika viwanja vya Chuo Kikuu cha Nairobi.</p>
<p>Lengo la tukio hilo ni kuamsha hamasa za wananachi wa Kenya katika Kongamano la Kijamii la Dunia. Kongamano la mwaka 2007 lilikosolewa kwa uwakilishi wa hali ya juu ya mashirika na vyama vya kimataifa na kiwango cha juu cha gharama ya usajili, na kuwaacha Wakenya wengi walio maskini kushindwa kuhudhuria. Wakenya waliofanya kazi ya kujitolea pia walilalamika kwa kutotendewa haki.</p>
<p>Kwa kutafakari, Oloo anasema kwamba kinachohitajika katika WSF ni uwakilishi mkubwa wa wanaharakati kutoka sekta ya wanajamii wenyewe kuliko mashirika yasiyo ya kiserikali.</p>
<p>“Wanaharakati wa kijamii kwa ujumla wana mtizamo wa kimaendeleo lakini sio wakati wote. Kwa mfano,  [nchini Kenya] tuna wanaharakati wa Mungiki ambao wana wanachama zaidi ya milioni. Wanafanya mambo mazuri lakini wakati mwingine wanajihusisha na vitendo vya kihuni, na wakati mwingine vya kihalifu. Kwa hiyo kikundi cha uanaharakati kwa namna moja au nyingine sio cha kimaendeleo, lakini vikundi vya kijamii ninavyoviongelea ni vile ambavyo vina mwelekeo wa kimaendeleo wa kuibadilisha jamii. Uanaharakati katika sekta zisizo rasmi, za wafanyakazi, vijana na wanawake – hivyo ndivyo vikundi ninavyoviongelea.”</p>
<p>Njoki Njehu ni miongoni mwa wanachama wa  <em>Daughters of Mumbi</em> <em>Resource Centre</em>, kituo cha mtandao wa vikundi vya wanawake vinavojitegemea vinavyofanya kazi katika masuala ya usalama wa chakula, haki za jinsia, ushiriki wa raia na demokrasia.</p>
<p>Njoki amekuwa akishiriki Kongamano la Kijamii Duniani tangu lilipoanzishwa katika mji wa Porto Alegre mwaka 2001 nchini Brazil. Njehu anakubali na ukweli kwamba hamasa ilipungua baada ya Kongamano la Kijamii la mwaka 2007, lakini anasema wanachama wa kikundi chao wamebadilisha mtazamo wa ushiriki katika kongamano la WSF litakalofanyika Nairobi.</p>
<p>“Walihamasishwa kuelewa kwamba ushindani ndio njia ya maisha. Haiyumkini kufikiri kwamba maisha ni ushindani wakati wote, kwa sababu mtu anapigania katika kujaribu kupata fedha kwa ajili ya mtoto, suala sio tu ni mtoto bali kupatikanaji wa elimu kwa watoto wote. Iwapo unapigania kupinga mtu anayevuta kinywaji haramu cha gongo (chang’aa)  au bangi katika jamii yako au hupati huduma muhimu kwa sababu una tatizo, kwa mtizamo huo basi sio tu kwa ajili yako, ni kwa ajili ya huduma na hali halisi katika jamii yako.”</p>
<p>Betty Makena Mutugi amekuwa mwenyekiti wa kamati ya wanawake katika Chama Kikuu cha Wafanyakazi  (COTU) kwa kipindi cha miaka minne iliyopita. Alijitahidi kusukuma ushiriki wa wanawake katika ngazi za uongozi kwa wanawake vijana na wenye umri mkubwa katika chama hicho, halikadhalika alipigania haki za mwanamke katika mahali pa kazi. Kongamano la Dakar litakuwa la kwanza kuhudhuriwa na Mutugi.</p>
<p>“Nilipoalikwa katika kongamano hili, nilijisikia vizuri upande wangu ili niweze kujitayarisha na kuona vikundi vingine vinafanya nini,” alisema. Mutugi atakuwa mwakilishi pekee kutoka COTU lakini atakutana na vikundi vingine vingi vya umoja wa wafanyakazi barani Afrika na hata kutoka nje, ambao watajiunga kwa pamoja kuongeza nguvu katika mapambano yao.</p>
<p>“Tuna tatizo kubwa la ubinafsishaji na serikali inachukuwa fursa hiyo, kwa kusema kwamba kuna tatizo au mgogoro. Na wakati wanabinafsisha makampuni hayo hutuambia kwamba itabidi pia wapunguzwe wafanyakazi, nendeni nyumbani, na mara wawekezaji wakiwasili na kununua kampuni, wanaleta watu wao.”</p>
<p>Mithika Mwenda ni mratibu wa shirika la <em>Pan-african Climate Justice Alliance</em>, ambalo ni miongoni mwa watayarishaji wa kongamano la awali la Kijamii la Dunia.</p>
<p>“Kama ujuavyo ni vigumu kwa kila mtu kushiriki. Hivyo basi tunajipanga kuhakikisha ni kwa kiasi gani tutakuwa na uwakilishi wa kutosha katika mchakato huu, sio lazima kwenda Dakar, lakini ule moyo wa kulitambua kongamano hilo. Pili, tunaamini kwamba Kongamano la Kijamii la Dunia ni fursa kubwa ya kurekebisha udhalimu uliokuwa ukitendeka dhidi ya watu kwa muda mrefu.”</p>
<p>Anasema kwamba mkutano wa Januari 29 umekonga nyoyo za harakati za kijamii kwa kuleta maelewano katika tofauti za kikabila zilizojitokeza nchini Kenya.</p>
<p>“Tulianza kwa kujiuliza wenyewe, sawa tunakwenda, lakini tunawahusishaje wenzetu katika ngazi ya kitaifa? Je, ni nini tunaenda kufanya?” alisema. “Hamasa za Kongamano la Kijamii la Dunia ni ushiriki wa watu. Ni kujaribu kuangalia ni kwa namna gani wazawa katika ngazi ya chini, jamii ya msituni na maskini, watu wenye ulemavu, vijana na wengine wote wanaweza kushiriki katika siasa za nchi yetu na hata katika ngazi ya kimataifa kwa ujumla.”</p>
<p>“Wakati Wakenya wanaelekea katika Kongamano la Kijamii la Dunia huko Dakar, wanatarajia kubadilishana uzoefu, na kurejea nyumbani na mikakati mipya na habari njema zenye matumaini ambazo tunaweza kuzichukua ili kufanikisha malengo yao kwa ajili ya kuboresha haki katika maisha ya jamii, kama kauli mbiu ya Kongamano la Kijamii la Dunia lisemavyo, “Dunia mpya inawezekana.”</p>
<p>(END/2011)</p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://www.ips.org/TV/wsf/kongamano-la-kijamii-la-dunia-wakenya-wanawasha-moto-mwingine/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Taasisi za Benki Zinashambuliwa, Bila Kujali</title>
		<link>http://www.ips.org/TV/wsf/taasisi-za-benki-zinashambuliwa-bila-kujali/</link>
		<comments>http://www.ips.org/TV/wsf/taasisi-za-benki-zinashambuliwa-bila-kujali/#comments</comments>
		<pubDate>Sun, 06 Feb 2011 22:11:46 +0000</pubDate>
		<dc:creator>editor</dc:creator>
				<category><![CDATA[Swahili]]></category>
		<category><![CDATA[WSF 2011]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://www.ips.org/TV/wsf/?p=2563</guid>
		<description><![CDATA[Kongamano la Uchumi la Dunia limekuwa uwanja wa watunza fedha katika mabenki mwaka huu kutafuta mbinu za kuendeleza utamaduni wake wa mamlaka.]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<p><a href="http://www.ips.org/TV/wsf/library/WEF.jpg"><img class="alignleft size-medium wp-image-2335" style="margin-top: 2px; margin-bottom: 2px; margin-left: 10px; margin-right: 10px;" title="WEF" src="http://www.ips.org/TV/wsf/library/WEF-300x208.jpg" alt="" width="300" height="208" /></a>Na<strong> </strong>Julio Godoy</p>
<p><strong>BERLIN, Feb 3, 2011 (IPS) – Kongamano la Uchumi la Dunia limekuwa uwanja wa watunza fedha katika mabenki mwaka huu kutafuta mbinu za kuendeleza utamaduni wake wa mamlaka. Na kwa mara nyingine, ulikuwa ulingo – tofauti na vile vile kupinga Kongamano la Kijamii la Dunia ambalo linatarajiwa kuanza wiki ijayo katika mji Mkuu wa Senegal, Dakar – ambako madhara makubwa ya utandawazi na yanayotokana na mazingira kutokana na ongezeko lisilozuilika liliachwa kando.<span id="more-2563"></span><br />
</strong><strong> </strong></p>
<p><strong> </strong></p>
<p>&#8220;Tulichokiona Davos ni malipo ya ridhaa yetu wenyewe ya mtaji wa shirika,&#8221; Rainer Falk, mtaalam wa uchumi wa utandawazi na mchapishaji wa jarida la wiki lijulikanalo kama ‘World Economy Development’ lililoko Luxembourg, ameliambia shirika la habari la IPS.</p>
<p>&#8220;Ni wazi kwamba mbali na madhara yanayoonekana kwa ajili ya utulivu kimataifa na utengamano katika jamii bado kuna msimamo wa fikra za matokeo ya muda mfupi ya kiuchumi katika Kongamano la Uchumi la Dunia (WEF) na mashirika makubwa ya fedha kwa ujumla,&#8221; Falk alisema.</p>
<p>Japokuwa WEF inadai kwamba ni mkusanyiko wa watu mashuhuri kiuchumi na kisiasa kutoka nchi zenye viwanda vikubwa, na kama ni hivyo kwa kutumia busara hizo kimataifa, ukweli uliopo ni kwamba ulingo huo haukuona mbali mgogoro wa kifedha na kiuchumi ulioikumba dunia hadi kusababisha madhara makubwa.</p>
<p>Mwaka huu WEF kwa mara nyingine lilipata mshtuko kutokana na uasi uliotumia nguvu katika nchi za Maghreb, ambao ulisababisha kuondolewa madarakani kwa Kiongozi wa Kidikteta wa Tunisia Zine El Abidine Ben Ali na kukaribia ukingoni mwa serikali la Hosni Mubarak wa Egypt.</p>
<p>Mbali na dosari hizo, WEF iliendelea na shughuli zake kama kawaida. Badala ya kuyakabili madhara yaliyotokana na kuporomoka kwa uchumi duniani, na kuhamasisha udhibiti wa kimataifa katika biashara zinazoshukiwa kuzorota, baadhi ya washiriki katika mkutano wa Swiss Alps walitoa wito wa kuacha kuzishambulia taasisi za benki.</p>
<p>Kwa mfano Dimon, Mtendaji Mkuu wa benki ya kitegauchumi ya JP Morgan, alisema kushambulia &#8220;si jambo zuri kulifanya.&#8221; Dimon aliiambia hadharahuko Davos kwamba ilikuwa ‘dhana kubwa ambayo haikuelewa’ kwamba mabenki yote yalikumbwa na kutokuwa na uwezo wa kulipa wakati huu wa mgogoro wa uchumi.</p>
<p>&#8220;Sio kwamba (mabenki yote ya vitegauchumi na fedha za kuzungusha) ziko sawa, sio kwamba watendaji wakuu wote wako sawa. Tunajaribu kufanya kinachowezekana kila siku,&#8221; alisema.</p>
<p>Dimon, pamoja na watendaji wakuu wengine wanaoongoza mabenki ya kimataifa, kimsingi walipinga pia marekebisho ya soko la fedha. &#8220;Naweza kuthibitisha uwezekano wa mabadiliko baada ya yaliyotokea,&#8221; Dimon alisema. &#8220;Lakini kushauri kwamba tunatakiwa kuinama na kukubali kwa sababu tunatunza fedha – hilo halikubaliki, sio haki.&#8221;</p>
<p>Mabenka waliohudhuria katika WEF huko Davos waliezea wasiwasi wao kuhusu mapungufu makubwa ya umma yanaweza kusababisha hali ya mgogoro wa kifedha kurudia tena, na kutoa wito kwa masharti makali katika mipango na kupunguza kwa kiasi kikubwa matumizi ya fedha za umma.</p>
<p>WEF halikadhalika unaendelea kupuuza matatizo ya kwamba kuongezeka kwa joto duniani kunaweza kusababisha kusitishwa kwa shughuli za kiuchumi. Badala ya kutoa vivutio kwa vyanzo vinavyobuni nishati na kufikiria mifano mbadala ya uchumi, mijadala ya WEF inagusia tu masuala ya ufanisi wa ekolojia kwa uchache sana.</p>
<p>Falk anasema kwamba WEF imeshindwa kuzungumzia masuala muhimu. &#8220;WEF limejitosheleza lenyewe na baadhi ya maneno kuhusu ufanisi wa ekolojia. Bila shaka, washiriki wengi katika mkutano huo wa  Davos aidha bado wanaamini kwamba kuongezeka kwa joto kunaweza kuzuiwa kwa kupunguza baadhi ya mifumo, au wanakwepa ukweli uliopo.&#8221;</p>
<p>Kerstin Sack, mratibu wa Kikundi cha ATTAC  kutoka Ujerumani, alisema kwamba WEF imeshindwa kufikia maazimio yanayohusu “matatizo muhimu ya maisha yetu, hususan uhaba wa chakula, ukiukwaji wa kijamii kimataifa na migogoro ya kimataifa inayohusiana na malighafi.&#8221;</p>
<p>Sack amesema kwamba kauli mbiu ya mkutano wa WEF mwaka huu imepotosha. Mkutano ulikusanyika chini ya bango lililoandikwa ‘Miongozo ya Pamoja kwa Dunia Mpya’. &#8220;Lakini watu waliofika katika mkutano huo Davos hawako tayari kukubali kwamba miongozo ninawafaa wote,&#8221; Sack ameliambia IPS.</p>
<p>Sack pia ameshutumu miito iliyotolewa na watendaji wakuu wa mashirika ya kimataifa benk za vitegauchumi na fedha zilizokusanywa huko Davos zimepunguza kwa kiasi kikubwa hasara kwa umma.</p>
<p>&#8220;Huu ni ukomo wa unafiki wa shirika,&#8221; Sack amesema.  &#8221;Viongozi hao hao wa makampuni walionusurika kuporomoka kutokana fedha za walipa kodi hivi sasa wanatoa wito wa kuongeza makato katika huduma za kijamii.&#8221;</p>
<p>Upuuzi wa WEF unapingana na mwelekeo wa kongamano jingine la kimataifa, hususan Kongamano la Kijamii la Dunia (WSF) – ambalo litaanza wiki ijayo katika mji mkuu wa Senegal, Dakar.</p>
<p>Wakati washiriki katika kongamano la WEF wanarudi katika shughuli zao za kawaida za sera, WSF itakuwa ikijadili masuala muhimu ambayo Watendaji Wakuu wa kongamano la Davos imedharau – nayo ni uhaba wa chakula, mabadiliko ya hali ya hewa na ukoloni mamboleo.</p>
<p>(END)</p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://www.ips.org/TV/wsf/taasisi-za-benki-zinashambuliwa-bila-kujali/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
	</channel>
</rss>
